Idara ya Sera na Mipango
JUKUMU KUU
Kutoa utaalam na huduma katika sera, mipango, maandalizi ya bajeti; na utafiti na uvumbuzi.
Idara ina Sehemu Mbili (2):
(i) Sehemu ya Sera, Utafiti na Ubunifu; na
(ii) Sehemu ya Mipango na Bajeti.
Idara inaongozwa na;

Bw. David Emmanuel Mwankenja
Mkurugenzi wa Idara Sera na Mipango (DPP)
Barua pepe: david.mwankenja@mawasiliano.go.tz
WASIFU WA BW.DAVID MWANKENJA.
Bw. David Emmanuel Mwankenja ni Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango katika Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari anauzoefu wa zaidi ya miaka 18 katika uchambuzi wa sera, upangaji wa maendeleo, usimamizi wa bajeti, na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo ya kitaifa.Kabla ya wadhifa huu, amehudumu kama Mkurugenzi Msaidizi katika Wizara ya Fedha na Mipango, Mchumi Mkuu katika Ofisi ya Rais – Tume ya Mipango, na Ofisi ya Rais – Kitengo cha Ufuatiliaji wa Utekelezaji (President’s Delivery Bureau), akishiriki kikamilifu katika maandalizi ya Mipango ya Maendeleo ya Miaka Mitano ya Taifa na Mpango wa Maendeleo wa Muda Mrefu wa Taifa (2011/12 – 2025/26).
Kielimu, Bw. Mwankenja alipata Shahada ya Kwanza ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Shahada ya Uzamili katika Sera za Maendeleo ya Kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Bradford, Uingereza. Aidha, amepata mafunzo katika uongozi na ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo kupitia taasisi za kitaifa na kimataifa.
Bw. Mwankenja ni mjumbe wa bodi katika taasisi kadhaa za umma ikiwemo Taasisi ya MOI na UTT-AMIS, na amewakilisha Tanzania katika mikutano mbalimbali ya kimataifa kuhusu maendeleo endelevu, uchumi na ushirikiano kati ya sekta ya umma na binafsi.
MAJUKUMU YA IDARA YA SERA NA MIPANGO
(i)Uratibu wa Mipango na Uundaji wa Sera kuratibu maandalizi ya mipango, bajeti na sera za wizara kwa kuzingatia mifumo ya mipango ya kitaifa.
(ii)Uchambuzi na Ushauri wa Sera kuchambua sera kutoka sekta nyingine na kutoa ushauri unaofaa.
(iii)Uratibu wa Utafiti kuratibu tafiti kuhusu sera za wizara na shughuli za sekta husika kwa ajili ya maendeleo ya sekta hiyo.
(iv)Utekelezaji wa Sera na Ubunifu wa Serikali kuratibu utekelezaji wa sera za Serikali, tafiti, maendeleo ya kiteknolojia na ubunifu ndani ya Wizara.
(v)Maandalizi ya Hotuba ya Bajeti kuratibu maandalizi ya Hotuba ya Bajeti ya Wizara.
(vi)Miongozo ya Utafiti na Ubunifu kuandaa miongozo kuhusu masuala ya utafiti na ubunifu kwa ajili ya Wizara.
(vii)Ufuatiliaji wa Utoaji Huduma kufanya Utafiti wa Utoaji Huduma wa Wizara.
(viii)Tathmini ya Ndani ya Wizara kuratibu Tathmini ya Kujipima ya Wizara (Tathmini ya Taasisi).
(ix)Uhamasishaji wa Rasilimali kuhamasisha rasilimali kwa ajili ya utekelezaji wa miradi na mikakati ya Wizara.
(x)Usimamizi wa Hatari kuratibu shughuli za usimamizi wa hatari ndani ya Wizara.
(xi)Utekelezaji wa Ilani ya Chama na Maelekezo ya Serikali kuratibu utekelezaji wa Ilani ya Chama Tawala, maelekezo ya Serikali na masuala ya Bunge.
(xii)Uandaaji wa Taarifa za Utendaji kuratibu maandalizi ya Taarifa za Utendaji za Kipindi kwa ajili ya Wizara.
