Kitengo cha Fedha
JUKUMU KUU
Kutoa huduma za usimamizi wa fedha na uwekaji hesabu kwa Wizara.
Kitengo cha Fedha na Hesabu kinaongozwa na;
Bi. Kezia Katamboi (CPA)
Kaimu Mhasibu Mkuu (CA).
Barua pepe: kezia.katamboi@mawasiliano.go.tz
WASIFU
MAJUKUMU YA KITENGO CHA FEDHA NA HESABU;
Ofisi ya Fedha
(i) Kuwasilisha orodha ya vocha Hazina;
(ii) Kukusanya hundi zote kutoka Hazina;
(iii) Fedha taslimu na hundi za benki;
(iv) Kutayarisha ripoti ya kila mwezi;
(v) Kulipa fedha taslimu/hundi kwa wafanyakazi/wateja (Mtoa huduma)
(vi) Hundi za malipo ya vocha;
(vii) Kutunza daftari la fedha,
(viii) Kutunza kumbukumbu za masurufu yote yaliyotolewa; na
(ix) Kutayarisha na kutekeleza malipo yote
Mapato
(i) Kukusanya mapato yote;
(ii) Kusimamia mapato kwa mujibu wa kanuni na miongozo;
(iii) Kukusanya kodi ya mwaka, ada za maombi na ada nyinginezo; na
(iv) Kufanya usuluhishi wa Benki.
Bajeti
(i) Kufuatilia mgao na matumizi; na
(ii) Kuandaa Hesabu za Mwisho na taarifa nyingine za fedha.
Kuhakiki na kukagua nyaraka na vocha zilizoidhinishwa kabla ya malipo
(i) Kuthibitisha nyaraka sahihi za kusaidia vocha ikiwa ni pamoja na idhini kulingana na kanuni;
(ii) Kuchunguza nyaraka za mwisho ili kuhakikisha uzingatiaji wa sheria husika, kanuni, waraka n.k; na
(iii) Kujibu hoja zote za Ukaguzi zilizoulizwa katika mwaka wa fedha uliopita.