Idara ya Mawasiliano
LENGO;
Kutoa utaalamu wa Sera, Mikakati na Miongozo ya Kitaifa ya maendeleo ya mawasiliano.
Idara ina Sehemu tatu (3): (i)Sehemu ya Uwekezaji wa Mawasiliano;
(ii) Sehemu ya Huduma za Mawasiliano na Utangazaji; na (iii) Sehemu ya Huduma za Posta.
Idara inaongozwa na;
Mkurugenzi wa Huduma za Mawasiliano (DC)
Email:
MAJUKUMU YA IDARA YA MAWASILIANO
(i) Kuanzisha, kutunga na kupitia sera za Mawasiliano, Mikakati na miongozo ya maendeleo ya sekta;
(ii)Kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera, mikakati na miongozo ya Mawasiliano,
(iii) Kuratibu utangazaji na matumizi ya bidhaa na huduma za Mawasiliano kwa maendeleo ya Taifa;
(iv) Kuratibu Huduma za Taifa za Mawasiliano ili kuwezesha sekta nyingine za uchumi;
(v) Kuweka mazingira mazuri ya kukuza uwekezaji katika sekta ya mawasiliano;
(vi) Kuimarisha upatikanaji na uwezo wa kumudu bidhaa na huduma za mawasiliano kwa umma;
(vii) Kukuza na kuwezesha utekelezaji wa majukumu ya Huduma za Mawasiliano kwa Wote;
(viii) Kukuza na kuwezesha maendeleo ya taasisi za huduma za mawasiliano;
(ix) Kusimamia mawasiliano ya Kikanda na Kimataifa katika dhamira ya kuharakisha ubia;
(x) Kuweka mifumo ifaayo inayokuza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika matumizi na usimamizi wa huduma za Mawasiliano; na
(xi) Kukuza ushindani katika utoaji wa huduma za mawasiliano kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
