Kitengo cha Mawasiliano Serikalini (GCU)
LENGO
Kutoa ushauri wa kitaaluma na huduma za habari, mawasiliano na midahalo na umma pamoja na vyombo vya habari
Kitengo kinaongozwa na;
Bi. Isabela Katondo
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini (HGCU)
Barua pepe: Isabela.katondo2@mawasiliano.go.tz
WASIFU
MAJUKUMU YA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
(i) Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa Mkakati wa Mawasiliano;
(ii) Kuratibu utayarishaji na urushaji wa vipindi maalum vya TV na redio;
(iii) Kuratibu uzalishaji na usambazaji wa matoleo maarufu ya sera, kanuni na miongozo ya Wizara;
(iv) Kutayarisha na kutekeleza kampeni za Uhamasishaji Umma kuhusu matumizi na programu za huduma na miundombinu ya TEHAMA;
(v) Kupangilia ufanyikaji wa mahojiano ya kuandaa vipindi maalum vya TV na redio kuhusu maendeleo ya Sekta ya TEHAMA;
(vi) Kuandaa na kusimamia uzalishaji na usambazaji wa taarifa, elimu na mawasiliano kwa ajili ya wadau wa Wizara;
(vii) Kukuza ufahamu wa majukumu ya wizara, programu, miradi na sera kwa wadau na umma kwa ujumla;
(viii) Kuandaa maudhui na kuchapisha kwenye tovuti ya wizara na mitandao ya kijamii kwa ajili ya matumizi ya umma na wadau;
(ix) Kuanzisha na kufuatilia taratibu za kupata mrejesho kutoka kwa wadau na umma kwa ujumla;
(x) Kuchapisha na kusambaza Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa Wizara;
(xi) Kuratibu utoaji wa taarifa kupitia vyombo vya habari wakati viongozi wa Wizara, wabunge na wadau wa Wizara wanashiriki katika mikutano, semina, warsha, uzinduzi, kutembelea maeneo ya miradi inayotekelezwa na Wizara mijini na vijijini;
(xii) Kuratibu taarifa za Wizara kwa Vyombo vya Habari ili kuongeza uelewa na uwajibikaji kwa wananchi; na
(xiii) Kuratibu na kusimamia ufuatiliaji wa kila siku kwenye machapisho, majukwaa ya kielektroniki na mitandao ya kijamii kuhusu masuala yanayohusu TEHAMA.