Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini
JUKUMU KUU
Kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera, Mpango Mkakati wa Muda wa Kati (MTEF), mipango ya mwaka, bajeti, programu na miradi iliyo chini ya Wizara
Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini kinaongozwa na;
Bw. Adam Mwaigoga
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini.
Email: adam.mwaigoga@mawasiliano.go.tz
WASIFU
MAJUKUMU YA KITENGO
(i) Kufuatilia na kutathmini Maeneo Muhimu ya Kitaifa ya Matokeo (NKRAs) kwa Wizara;
(ii) Kufanya tathmini ya athari za muda mrefu kwenye mipango, programu na miradi iliyo chini ya Wizara;
(iii) Kuandaa na Kutekeleza Muundo na Mfumo wa U&T wa Wizara;
(iv) Kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo ya tathmini;
(v) Kutayarisha Taarifa za mara kwa mara za U&T kuhusu NKRAs chini ya Wizara;
(vi) Kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Ilani ya Chama Tawala na maagizo ya Serikali;
(vii) Kufuatilia na kutathmini utendaji wa muda na tathmini za mara kwa mara za Wizara;
(ix) Kufuatilia utendaji wa taasisi zilizo chini ya Wizara;
(x) Kuratibu mapitio ya utendaji Kitaasisi/ Mfumo wa Taarifa za Utendaji wa Taasisi za Umma (PIPMIS); na
(xi) Kuwa mwangalizi wa Takwimu za Wizara.