Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Kitengo cha Usalama wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

KITENGO CHA USALAMA WA MAWASILIANO NA MTANDAO

LENGO
Kuwa na mazingira salama ya kusaidia matumizi ya mawasiliano, Bidhaa na Huduma za ICT.

Kitengo kinaongozwa na;

Mhandisi Stephen Mwita Wangwe

Mkurugenzi wa Usalama wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Barua pepe; stephen.wangwe@mawasiliano.go.tz

WASIFU

Mhandisi Stephen Mwita Wangwe ni Mkurugenzi wa Usalama wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari. Mhandisi Wangwe ana uzoefu katika nyanja wa usalama wa mtandao kwa zaidi ya miaka 15 kati ya hiyo, miaka 6 amehudumu katika nafasi za uongozi ndani ya tasnia ya usalama wa mtandao.

Mhandisi Wangwe ni mhandisi aliyesajiliwa katika nyanja ya Uhandisi wa Kielektroniki na Mawasiliano, na amebobea katika Usimamizi wa Miradi mbalimbali vilevile ana ujuzi mahususi katika eneo la usalama wa mtandao. Miongoni mwa majukumu aliyofanikisha katika utendaji wake ni pamoja na kushiriki moja kwa moja katika maandalizi ya Mkataba wa Umoja wa Afrika (AU) juu ya Usalama wa Usalama na Ulinzi wa Takwimu za Kibinafsi (Malabo Convention) wa mwaka 2014 na Sheria za mfano za Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) juu ya Usalama Mtandaoni za mwaka 2010; Uridhiwaji wa Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ya Mitandao ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA); Kubuni na kusimamia miradi mbalimbali ikiwemo Shule Mtandao, Sheria za Usalama wa Mtandao, Haki Mtandao, Muundombinu wa Taifa wa Saini Salama za Kielektroniki (NPKI) na Uendeshaji wa Mikutano kwa njia ya Video; Amekuwa Mwakilishi wa Taifa katika Timu ya Majadiliano ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa kukabiliana na matumizi ya TEHAMA kwa madhumuni ya kutekeleza jinai; Mwongozo kwa Taasisi zinazohusika na Kupambana na Uhalifu wa Mtandao nchini; Mkakati wa Taifa wa Usalama Mtandao (2018 - 2023); Mkakati wa Taifa wa Elimu kwa Umma kuhusu Usalama wa Mtandao (2021/2022 - 2025/2026); Orodha ya Kitaifa ya Miundombinu Muhimu ya TEHAMA (CII) pamoja na miongozo ya utambuzi, usimamizi wa vihatarishi, ukaguzi na usimamizi wa jumla  wa Miundombinu hiyo;  Nyaraka za Kitaasisi ikiwa ni pamoja  na Mipango ya Upatikanaji wa Huduma wakati wote (BCPs), Mipango ya Urejeshaji wa Huduma wakati wa Maafa (DRPs) na  Sera ya TEHAMA; na kufanikisha utungwaji wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, Sheria ya Miamala ya Kielektroniki ya mwaka 2015 na hivi karibuni Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya mwaka 2022 pamoja na kanuni zake.

Kwa uzoefu wake mkubwa Mhandisi Wangwe ana maono ya kuiwezesha nchi yetu kuwa na anga ya mtandao inayoaminika. Aidha, Mhandisi Wangwe ana shauku ya kuipandisha nafasi Tanzania Kikanda na Kimataifa katika masuala ya usalama mtandao kwa mujibu wa viwango na vigezo vilivyowekwa na kukubalika Kimataifa.

 


MAJUKUMU YA KITENGO CHA USALAMA WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI

(i) Kuandaa sera, sheria, mkakati, miongozo na kanuni zinazohusiana na Usalama na Usalama wa mawasiliano na teknolojia ya habari;

(ii) Kuanzisha utaratibu sahihi wa kuwezesha utekelezaji wa usimamizi wa usalama wa mawasiliano nchini;

(iii) Kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera za usalama wa mawasiliano na teknolojia ya habari,

(iv) Kuweka mazingira sahihi ya kuwezesha utekelezaji wa hatua za kuzuia uhalifu wa kimtandao nchini;

(v) Kuratibu maendeleo ya mikakati na mpango wa kukuza usalama wa vifaa vya teknolojia ya mawasiliano.

(vi) Kuratibu maendeleo ya mikakati na mpango wa kukuza mwendelezo wa Biashara na uzuiaji wa majanga mbalimbali ya usalama wa mawasiliano;

(vii) Kukuza mipango ya teknolojia ya mawasiliano; Na

(viii) Kufanya ukaguzi wa mifumo ya Tehama ili kuhakikisha kuwa inaendana na mahitaji ya usalama wa mawasiliano.