Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Habari

WADAU TOENI MAONI CHANYA YA TEHAMA


Na Chedaiwe Msuya, WHMTH, Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu  wa Wizara ya Habari Mawasiliano na Teknolojia,  Selestin Kakele amesema watu  watoe maoni chanya katika matumizi ya TEHAMA ili kuboresha maisha ya watanzania katika ulimwengu wa kidigitali. 

Hayo amebainisha leo Septemba 27 jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu huyo wakati akifungua kikao  cha kutoa maoni kuhusu ya sera ya Taifa ya TEHAMA  kwaajili ya makundi Anuai amesema  hichi wanachofanya wataendelea kwa makundi mengine.

Amesema wizara zote  ni kutunga na kusimamia sera,  kanuni, miongozo na sheria ambayo huwa inasimamia utekelezaji wa majukumu wizara wanatekeleza wajibu   wa msingi.

"Sera ya TEHAMA  ya mwaka 2016 ni mda mrefu  umepita na TEHAMA  na kama kiumbe ambacho kinazaliwa  kinakua na kinabadilika kulingana  na wakati na mambo mbalimbali  yanatokea duniani katika jamii,"amesema Kakele.

Amesema wakati wanatunga sera hiyo  mwaka 2016 hakukuwa na mambo ambayo leo yanatokea hatakama yalikuwepo hakuana mtu angeweza kufasihi miaka michache ambacho kinatokea leo ingekua je?.

Amesema Teknolojia inakua  kwa kasi sana ipo haja  ya kufanya marejeo ya sera ya TEHAMA zipo taratibu za kuandaa sera  moja ya shariti la msingi ni ushirikwishaji wa jamii.

"Tumekuwa na utaratibu huu tangu tunaanza mchakato  wa kukutana na makundi mbalimbali na leo tumeona tukutane na makundi Anuai wenye changamoto mbalimbali za  ulemavu lakini ni wadau wetu muhimu katika sera  tunajaribu kuifanyia mapitio,"amesema. 

Aidha  amesema  wanataka sera hiyo watakuwa wamekubaliana na kukamilika itumike kujibu changamoto na kuwasaidia kutoa majawabu changamoto zinazowakabili watu kwenye makundi anuai katika mlengo wa TEHAMA. 

Ameongeza kuwa watawezeshaje taasisi za serikali na sekta binafsi  zinakihusisha na TEHAMA kuzingatia mahitaji maalumu katika utoaji huduma zao.

Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama  Watu Wenye Ulemavu Nchini(SHIVAWATA), Ernest Kimaya amesema sera ya TEHAMA ni muhimu kwa watu wenye ulemavu kutoa maoni  kuboresha sera.

Naye Afisa Habari  Chama cha Wachimbaji  Wanawake Madini, Halima Mhando amesema hakuna  maendeleo yeyote  bila mawasiliano  kwa sasa  hakuna kitu kinafanyika  bila TEHAMA  watatoa maoni yenye tija.

Kikao hicho kiliweza kuhudhuriwa na Bw.  Mohamed Mashaka Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Mifumo na Huduma za TEHAMA (DISDS), Mratibu wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali,Bw.Baraka pamoja na baadhi wa viongozi wa Wizara.