Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Habari

MHE. MAHUNDI AKUTANA NA WAZIRI WA SAYANSI NA TEKNOLOJIA WA SERIKALI YA ZAMBIA


Na Mwandishi Wetu, WHMTH, Zambia

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) amekutana na kuzungumza na Waziri wa Sayansi na Teknolojia  wa Serikali ya Zambia, Mhe. Felix Mutati tarehe 3 Oktoba, 2024.

Katika kikao hicho Mhe. Mahundi pamoja na mwenyekiti wake wamejadili masuala mbalimbali kuhusu Sekta ya Mawasiliano katika Nchi hizo mbili na kuangalia maeneo ambayo Serikali ya Tanzania inaweza kushirikiana na Serikali ya Zambia  kuleta maendeleo chanya kwa Nchi zote mbili. 
    
Mhe. Mahundi yupo Nchini Zambia kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Mawaziri wa Afrika kuhusu Serikali Mtandao (Digital Government Africa) ulio anza tarehe  2 na utamalizika tarehe 4 Oktoba 2024. ‎